Thursday, May 11, 2017

Trump: Sichunguzwi na FBI

Rais Trump anasema kuwa hachunguzwi
Rais Trump anasema kuwa hachunguzwi
 
Rais wa Marekani Donald Trump amesisitiza kwamba hafanyiwi uchunguzi wowote baada ya kumfuta kazi mkurugenzi wa shirika la ujasusi la FBI.
Bwana Trump aliambia chombo cha habari cha NBC kwamba ilikuwa uamuzi wake pekee kumsimamisha kazi James Comey.
Bwana Comey alikuwa akiongoza uchunguzi kuhusu madai ya Urusi kuingilia uchaguzi wa Marekani uliokamilika mbali na uwezekano kwamba kulikuwa na mawasiliano kati ya, maafisa wa Trump na Urusi wakati wa kampeni.
Bwana Trump ameutaja uchunguzi huo kuwa unafiki mkubwa madai yaliopingwa na Mrithi wa Comey.
Katika mahojiano yake ya kwanza tangu alipomfuta kazi mkurugenzi huyo , Bwana Trump aliambia NBC siku ya Alhamisi kwamba alimuuliza bwana Comey iwapo alikuwa akimchunguza.
Nilimwambia iwapo inawezekana unaweza kuniambia, Je Ninachunguzwa? Aliniambia ,huchunguzwi.
''Najua sichunguzwi'', Bwana Trump alimwamabia aliyekuwa akimhoji, akirejelea madai aliyotoa katika baraua ya Jumanne ya kumfuta kazi bwana Comey.
Rais huyo pia alipinga maelelezo ya ikuu ya Whitehouse kwamba alimfuta bwana Comey baada mapendekezo kutoka maafisa wakuu wa wizara ya haki.

Mugabe huwa anapumzisha macho si kulala

Bw Mugabe akiwa mkutanoni Afrika Kusini wiki iliyopita
Bw Mugabe akiwa mkutanoni Afrika Kusini wiki iliyopita
 
Msemaji wa Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe amesema kiongozi huyo huwa anapumzisha macho tu na si kulala wakati wa mikutano kama wanavyoamini watu wengi.
Kiongozi huyo amekuwa akionekana kusinzia katika mikutano mingi.
"Rais huwa anasumbuliwa na mwanga mkali," George Charamba amenukuliwa akisema na gazeti la serikali la Herald.
Rais huyo kwa sasa yupo nchini Singapore akipokea matibabu maalum kwenye macho yake.
Bw Mugabe, 93, anapanga kuwania tena urais katika uchaguzi mkuu mwaka ujao.
"Huwa najihisi kama mtu ambaye amekosa kutekeleza kazi yake vyema ninaposoma (kwenye vyombo vya habari na mtandaoni) kwamba rais alikuwa anasinzia katika makongamano - la hasha," Bw Charamba amesema.
Alilinganisha tatizo la Bw Mugabe na matatizo ya macho ambayo yalikuwa yanamsibu Rais wa zamani wa Afrika Kusini Nelson Mandela.
Bw Mandela alikuwa anatatizwa na mwanga mkali na wapiga picha hawakuruhusiwa kutumia mwanga wa kamera wakati wanapiga picha katika hafla zake.
Matatizo ya Bw Mandela yalitokana na kufanya kazi kwa muda mrefu katika timbo na pia kufungwa jela muda mrefu Robben Island.
Mugabe Bamako Januari 13, 2017.
Macho ya Robert Mugabe hutatizwa na mwanga, msemaji wake amesema. Hapa Mugabe anaonekana akiwa Bamako Januari 13, 2017.
Safari za Bw Mugabe za mara kwa mara nje ya nchi zimekuwa zikishutumiwa sana na wakosoaji wake.
Sekta ya afya nchini Zimbabwe imedorora na wahudumu wa afya hulalamika kwamba huwa hawalipwi vyema.

Dawa za kupunguza makali ya HIV zaboreshwa

Dawa za kupunguza makali ya Ukimwi
Dawa za kupunguza makali ya Ukimwi
 
Watafiti nchini Uingereza wanasema dawa za kupunguza makali ya virusi katika Ulaya na Amerika ya Kaskazini zimeboreshwa kiasi kwamba watu mwenye Virusi vya UKIMWI wanaweza kuishi kwa karibia sawa tu na watu wengine wasio na virusi.
Wanasayansi kutoka Chuo kikuu cha Bristol, waliwachunguza watu wenye virusi vinavyosababisha UKIMWI wapatao elfu tisini. Makadirio yao yanaonesha kuwa mtu mwenye umri wa miaka 21 aliyeanza matibabu mwaka 2008 au baadaye anaweza kuishi mpaka kufikia umri wake wa miaka 70.
Zaidi ya watu milioni mbili wanaishi na Virusi vya UKIMWI katika Ulaya na Amerika Kaskazini.
Kwa upande wa Takwimu za ulimwengu, watu walioathirika na virusi hivyo ni milioni 36 wengi wao wakiwa barani Afrika.

Source:YoungConcious

Majaribio ya ndege mpya za Boeing yasitishwa


Boeing 737 MAX
Shirika la ndege la Boeing limesitisha kwa muda safari za kufanyia majaribio ndege yake mpya ya 737 MAX kutokana na uwezekano wa kasoro kwenye injini za ndege hizo.
Hatua hiyo imechukuliwa siku chache kabla ya shirika hilo la ndege lenye makao yake Marekani kuwasilisha ndege za kwanza kwa mteja.
Lakini Boeing wamesema wataendelea na mpango wake wa kuanza kuwasilisha ndege hizo za MAX kwa wateja baadaye mwezi huu, na kwamba kampuni hiyo itaendelea kuunga ndege hizo kama kawaida.
American Airlines, Southwest, na shirika la Shandong Airlines la China ni miongoni mwa mashirika ambayo yameagiza ndege hizo.
Mapema mwaka huu, shirika la ndege la SpiceJet kutoka India liliwasilisha ombi la kununua ndege 205 mpya kutoka wka Boeing, ununuzi huo ukitarajiwa kuwa wa thamani ya $22bn (£18bn). Boeing wamesema ndege za kwanza za Max 737 zitawasilishwa kwa SpiceJet mwaka 2018.
Ndege za MAX zimeundwa kutotumia sana mafuta na zimeundwa kuchukua nafasi za ndege muundo wa 737 za awali, ambazo ziliuzwa kwa wingi sana na kampuni hiyo.
Boeing wanasema walifahamishwa wiki iliyopita kwamba huenda kuna kasoro kwenye injini za ndege hizo ambazo zilitengenezwa na kampuni ya kimataifa ya kuunda sehemu za injini ya CFM International.
CFM ni kampuni inayomilikiwa kwa pamoja na kampuni ya Marekani ya General Electric (GE) Safran ya Ufaransa na ndiyo iliyopewa kazi ya kuunda injini za ndege hizo za 737 Max.
Boeing wamesema hawakuwa wamepata taarifa zozote za hitilafu kwenye injini awali wakati was aa 2,000 za safari za majaribio.
Boeing 737 Max 9 taking off
Boeing 737 MAX 9 ilifanya safari yake ya kwanza Aprili
 
Ndege hiyo ya 737 MAX 8, inauzwa $110m lakini mashirika mengi ya ndege sana hupokea kipunguzo cha bei.
Muundo utakaofuata wa ndege hizo, 737 MAX 9, utakuwa na uwezo wa kubeba abiria wengi.
Kampuni ya Boeing ilisherehekea miaka 100 tangu kuanzishwa kwake mwaka jana.

Source:BBCSwahili

Mambo 9 kurudisha Soko la ya Kuzingatia Filamu Bongo


Muigizaji wa filamu za Bongo Elizabeth Michael ‘Lulu’.

 MAYASA MARIWATA | AMANI | MAKALA

KUTOKANA na wasanii wa fi lamu za Kibongo kuwa kwenye mikakati mizito ya kuhakikisha soko la kazi zao linarejea kwenye ubora wake kwa madai kuwa filamu za nje zimeua soko la ndani, kuna haja ya kuyazingatia haya yanayochangia kufeli kwao ili kupaa na kufi kia levo ya kimataifa.
Muigizaji wa Filamu, Kajala Masanja.
  1. UBORA WA STORI
Ninapozungumzia ubora wa stori moja kwa moja nawalenga waandishi wa script, unakuta mtu unaamua kuangalia filamu kwa bashasha ukiamini ‘utainjoi’ lakini mambo yanakuwa tofauti, unaitabiri fi lamu mwanzo mwisho na kweli itaenda hivyo.
Mfano unaweza ukasema hapo si kamsaidia lazima atamtongoza na kweli itakuwa hivyo, hapo ataingia chumbani kujifi cha basi itakuwa hivyo, unaweza ukakuta fi lamu nzima itaenda vile unavyohisi utadhani wewe ndiyo umeiandika, tofauti kidogo na fi lamu za wenzetu wanajitahidi kucheza na akili ya kawaida ya binadamu.
                   Staa wa muziki wa mduara na sinema za Kibongo, Snura Mushi.
  1. KURUDIA STORI
Kuna stori ambazo zimerudiwa `idea’ aidha kwa msanii mmoja au wasanii tofauti kuiga kazi ya mwenzao, mfano kuna fi lamu ya kaka mkubwa Vincent Kigosi `Ray’ aliicheza miaka ya nyuma, yeye ni mtoto wa tajiri lakini aliamua kuishi kimaskini na kwenda kufanya kazi kwenye nyumba ya matajiri kisha mtoto wa bosi akampenda.
Cha kustaajabisha siku chache zilizopita katoa fi lamu ya kufanana na hiyo ya Geat Keeper na yenyewe, Ray baba yake ni tajiri lakini yeye kaamua kuishi kimaskini na kwenda kufanya kazi nyumba ya matajiri na mwisho motto wa bosi akampenda na kuwa naye, swala hili pia linapunguza mvuto kwa mashabiki.
Muigizaji Bongo movie, Jenifer kyaka aka Odama.
  1. KUJUANA
Kuna tabia ambayo inafanywa na wasanii wengi ambayo hata baadhi yao wamekuwa wakilalamikia jambo hilo kuua soko, yaani msanii anavutiwa na muonekano wa mtu f’lani na kuamua kumchezesha kwenye fi lamu yake bila kumfanyisha mazoezi zaidi ya kumpa script aisome basi, matokeo yake anajikuta ‘akimbwela’ kwenye kamera na kuwafanya hata watazamaji wamshtukie na kuchukizwa naye.
Staa mwenye Bongo Muvi, Jacqueline Wolper Massawe.
  1. MAMBO YA KIZUNGU
Jambo hili linawahusu sana upande wa akina dada, unatazama fi lamu unaandikiwa miaka mitatu nyuma au mbele lakini cha kushangaza nywele ni zilezile zikiwa kwenye msuko uleule tena nywele za bandia, rasta au wigi, wakati nywele hizo haziwezi kusukwa miaka mitatu bila kufumuliwa, ina maana ni uongo wa wazi, pia usiku mtu kalala lakini kajazwa ‘make up’ si sawa.

  1. KUENDEKEZA UFUSKA
Muda mwingine ubora wa kazi unatoweka kutokana na tabia ya kuendekeza ufuska ‘ngono’ mida ya kazi, wasanii wengi wanapenda kukaa kambini lakini wakifika huko baada ya kuwaza kazi wanawaza mapenzi, hapo utasikia f’lani katoka na f’lani, huyu kamuibia mpenzi yule, basi balaa juu ya balaa matokeo yake muda wa kazi ukifi ka watu wanafanya ilimradi tu siyo kwa kiwango kile walichokikusudia.
Vincent Kigosi ‘Ray’.
  1. WIVU WA MAENDELEO
Inapotokea msanii kawa juu kuliko mwingine baada ya kuungana na mwenzao ili aweze kufanya vyema zaidi, wanaanza kumjengea chuki na kufanya njama za kumdidimiza, kama wasanii wakongwe kuna msanii anaibuka kwa kishindo basi mpeni sapoti ili afike mbali zaidi huenda akawavuta na nyinyi mkatoboa kupitia yeye.
  1. UNAFIKI
Kitendo ambacho naweza kusema kinairudisha nyuma tasnia kwa kiasi kikubwa ni hiki, baadhi ya wasanii wanawaza kufi tinishana muda wote yaani hiyo ni moja ya starehe kwao, mtu akiona f’lani na f’lani wanaelewana anawaza kuwachonganisha au wamekaa wanaongea vizuri mmoja akiinuka tayari mwingine anampiga majungu yaani upendo wa kweli ziro.
  1. USTAA
Kufanya kazi kwa kujiona ni mastaa f’lani kama vile Jacqueline Wolper, Wema Sepetu, Aunt Ezekiel, Jacob Steven ‘JB’, Chuchu Hans, Daudi Michael `Duma’ na wengine hii inachangia kupoteza ubora, sababu baada ya kuwa makini na unachokifanya unawaza tu mimi ni staa f’lani nitatazamwa tu, kazi yangu itauzika tu, siku hizi watu wameeilimika hawajali ustaa wa mtu wanachojali ni ubora wa kazi.
  1. KUTHUBUTU NA KUJIAMINI
Hili ni jambo la mwisho na la muhimu sana katika kuipeperusha vyema bendera ya nchi yetu, ondokaneni na nidhamu ya uoga changamkeni kutafuta chaneli ya kufanya kazi na wasanii wa nchi mbalimbali, ili kukuza soko letu na kuzidi kuipa sifa nchi yetu, tukaondokana na ile dhana kwamba fi lamu za Nigeria zinapendwa zaidi au za Kihindi au za Kizungu, kwa nini isiwe za Kibongo?


Source:GlobaPublishersTZ

Afrika yapewa nafasi 9 kombe la dunia 2026

Yaya Toure anayeichezea Manchester City ameshiriki katika kila mechi ambayo Ivory Coast imecheza katika michuano mitatau ya kombe la dunia
Yaya Toure anayeichezea Manchester City ameshiriki katika kila mechi ambayo Ivory Coast imecheza katika michuano mitatau ya kombe la dunia
Baraza la shirikisho la soka duniani Fifa limeidhinisha mpango wa kulipatia bara la Afrika nafasi 9 wakati kombe la dunia litakapoongeza timu zitakazoshiriki katika kinyanganyiro hicho na kufikia 48, 2026.
Hatua hiyo ilithibitishwa siku ya Jumanne mjini Bahrain. Kwa sasa bara hilo lina nafasi 5 pekee.
Taifa la kumi la Afrika litashiriki katika mchuano wa muondoano utakaojumuisha mataifa sita ili kuamua kuhusu nafasi mbili.
Baraza la Fifa lilipendekeza vile litakavyotoa nafasi hizo 48 mnamo tarehe 30 mwezi Machi.
Kinyang'anyiro hicho kipya kitashirikisha timu 16 kutoka Ulaya.
Wanachama wa Fifa walipiga kura mnamo mwezi Januari kuongeza timu zitakazoshiriki kutoka 32 hadi 48 kuanzia dimba la mwaka 2026.

 Source:BBCSwahili

Umesikia hii kuhusu Hisa za Snapchat kushuka

Mtandao wa Snapchat
Mtandao wa Snapchat
 
Hisa za mtandao wa Snapchat zimeshuka baada ya ripoti ya ukuaji mdogo katika kipindi cha miezi mitatu ya kwanza mwaka huu.
Katika matokeo yake ya kwanza tangu hisa hizo ziwekwe katika soko la hisa ,snachat imesema kuwa wateja wake wa kila siku waliongezeka asilimia 5 pekee na kufikia milioni 166 ikilinganishwa na kipindi cha miezi mitatu ya mwisho 2016.
Idadi hiyo ni milioni 2 chini ya ilivyotarajiwa, lakini ni ya juu kwa asimilia 36 ikilinganishwa na kipindi kama hicho mwaka uliopita.
Habari hizo zilisababisha hisa kushuka kwa asilimia 20 baada ya biashara mjini New York.
 
Ripoti ya Snapchat
Ripoti ya Snapchat
Wawekezaji hawakutarajia mapato ya juu na walihisi kukatika tamaa.
Hasara kubwa, ukuwaji mbaya na ishara hafifu kwamba mtandao huo hauna chochte cha kuvutia ili kukabiliana na ushindani wa mtandao facebook.
Mkurugenzi mkuu wa Snapchat Evan Spiegel alisema kuwa wateja wake wachache wa kila siku sio wasumbufu.

Source:BBCSwahili

Trump: Sichunguzwi na FBI

Rais Trump anasema kuwa hachunguzwi   Rais wa Marekani Donald Trump amesisitiza kwa...